Monday, August 30, 2010

Kanye & Jay-Z joint album




Hip-hop star Kanye West has announced a collaboration album with rap mogul Jay-Z. The controversial star tweeted about the upcoming five-song record.

More:

Jay-Z is married to this R&B diva.

West sparked controversy when he appeared on the cover of Rolling Stone in 2006.

At last year's MTV VMA Awards, West interrupted this country sweetheart's acceptance speech.

Liverpool yamsajili Raul Meireles








Klabu ya Liverpool imeimarisha sehemu ya kiungo baada ya kufanikiwa kumsajili Raul Meireles kutoka Porto ya Ureno.

Liverpool imelipa euro milioni 14 sawa na paundi milioni 11.5 za Uingereza kuweza kumnasa mchezaji huyo wa kimataifa wa Ureno mwenye umri wa miaka 27 aliyekwishacheza mechi 38 za kimataifa.

Mchezaji huyo mwenye nguvu sehemu ya kiungo anaonekana ataziba ipasavyo pengo lililoachwa na Javier Mascherano anayekamilisha harakati za kuhamia Barcelena.

Meireles amesema meneja wa Liverpool Roy Hodgson amefanya kazi kubwa kuweza kumsajili na kwake ni hiyo historia kubwa kujiunga na Liverpool.

Ameeendelea kusema ilikuwa ni ndoto yake ya siku nyingi kucheza ligi ya England na sasa ndoto hiyo imetimia.

Meireles anaungana na akina Milan Jovanovic, Joe Cole, Christian Poulsen, Jonjo Shelvey na Danny Wilson waliojiunga na Liverpool msimu huu.

Kiungo huyo aliichezea Ureno mechi zote nne nchini Afrika Kusini katika fainali za Kombe la Dunia mwaka huu.

Katika miaka yake sita aliyoichezea Porto mchezaji huyo wa zamani wa klabu za Boavista na Aves amefanikiwa kushinda mara nne ubingwa wa ligi ya Ureno.

Chelsea yazidi kuongoza England










Didier Drogba

Didier Drogba

Chelsea vinara wa Ligi Kuu ya England wameendeleza rekodi ya ushindi kwa msimu huu baada ya kuwalaza Stoke City mabao 2-0.

Pamoja na ushindi huo Chelsea walikosa kufunga mkwaju wa penalti baada ya Frank Lampard aliyecheza chini ya kiwango kupiga shuti hafifu lililodakwa na mlinda mlango Thomas Sorensen wa Stoke City.

Mabao ya Chelsea yalifungwa na Florent Malouda kipindi cha kwanza na bao la pili lilipachikwa na Didier Drogba kwa mkwaju wa penalti kipindi cha pili. Kwa matokeo hayo Chelsea wamefikisha pointi tisa kwa michezo mitatu na wanaongoza ligi hiyo.

Katika pambano lililochezwa mchana, Arsenal nao waliweza kujiongezea pointi tatu baada ya kuwafunga Blackburn Rovers nyumbani kwao mabao 2-1 na kufikisha ponti saba.

Matokeo mengine kwa michezo ya leo ya Ligi Kuu ya England, Blackpool walitoka sare ya kufungana mabao 2-2 na Fulham, Tottenham walikubali kipigo cha bao moja nyumbani kwao dhidi ya Wigan na Wolves walikwenda sare ya bao 1-1 walipowakaribisha Newcastle

Mascherano avutiwa na Barcelona









Liverpool imemuuza mcheza kiungo Javier Mascherano aliyepania kujiunga na klabu ya Uhispania Barcelona kwa takriban pauni milioni 17.25 imefahamishwa BBC.
Javier Mascherano

Mascherano sasa kuichezea Barcelona

Hata hivyo mpango mzima wa usajili utategemea mchezaji huyo ambaye ni nahodha wa timu ya taifa ya Argentina kufanikiwa majaribio ya afya huko Barcelona.

Klabu ya Barcelona imethibitisha kwenye tovuti yao kwamba vilabu vimeafikiana juu ya usajili wa Mascherano kwa kipindi cha misimu minne ijayo.

Pindi majaribio yakifanikiwa Barcelona itawafahamisha wakuu wa Liverpool na hivyo kukamilisha usajili.

Taarifa ya Barcelona imeongezea kusema kuwa mpango mzima wa usajili ulikamilishwa baada ya juhudi zilizofanywa na klabu katika dakika za mwisho ambapo mchezaji mwenyewe alishiriki majadiliano.

Inatazamiwa kuwa Mascherano atawasili huko Barcelona mwishoni mwa juma hili.

Katika mpango mzima Liverpool ilitaka irudishe pauni milioni 18 ilizolipa kumsajili mchezaji huyo alipowasili kutoka klabu ya West Ham.

Kabla ya hapo Liverpool ilikataa malipo ya pauni milioni 16 zilizopendekezwa na Barcelona siku saba zilizopita.

Hata hivyo hakushiriki mechi kati ya Manchester City na Liverepool

Thursday, August 26, 2010

Arsenal yamsajili Squillaci




Sebastian Squillaci

Klabu ya Arsenal imekamilisha taratibu za kumsajili mlinzi wa kimataifa wa Ufaransa Sebastian Squillaci kutoka klabu ya Sevilla.
Mlinzi huyo mwenye umri wa miaka 30 mwishoni mwa wiki iliyopita aliwasili London ambako alipimwa afya yake siku ya Jumatatu katika uwanja wa Emirates.

Mlinzi huyo wa kati wa zamani wa klabu ya Lyon ya Ufaransa hatacheza mchezo wa Jumamosi wa ligi dhidi ya Blackburn, lakini anaruhusiwa kucheza michezo ya ligi kuwania ubingwa wa vilabu vya Ulaya.

Squillaci anaonekana ataisaidia ngome ya Arsenal wakati huu walinzi wakongwe Sol Campbell, William Gallas na Mikael Silvestre wakiwa wameondoka katika klabu hiyo.

Imelezwa Arsenal imempatia mkataba wa miaka mitatu, licha ya kawaida ya Wenger kuwapatia mkataba wa muda mfupi wachezaji waliovuka umri wa miaka 30.

Mlinzi huyo alijiunga na Sevilla akitokea klabu ya Les Gones miaka miwili iliyopita na aliomba asichezeshwe katika mchezo wa marudio kutafuta nafasi ya kushiriki hatua ya makundi wiki iliyopita kati ya Sevilla na Braga ili asikose aweze kuichezea Arsenal katika mashindano hayo.

Wakati huu mlinzi mwengine wa Arsenal Philippe Senderos akiwa amehamia Evarton, Wenger alimsajili mlinzi wa kati Laurent Koscienly, ambapo kwa sasa klabu hiyo itakuwa na hazina kubwa ya walinzi wa kati baada ya Djourou naye kupona kabisa.
Squillaci alikuwemo katika kikosi cha ajabu ajabu cha Ufaransa kilichoshiriki Kombe la Dunia nchini Afrika Kusini na alicheza walipofungwa na wenyeji Bafana Bafana, hali iliyosababisha wamalize wa mwisho katika kundi lao.


Wakati alipokuwa majeruhi, aliweza kuanza kucheza mechi 14 za ligi kwa timu yake ya Sevilla msimu uliopita




Redknapp asema haogopi timu yoyote


Meneja wa Tottenham Harry Redknapp amesema wapo tayari kukabiliana na timu yoyote katika hatua ya makundi kuwania Ubingwa wa Ulaya.

Spurs iliilaza Young Boys mabao 4-0 pambano lililochezwa uwanja wa White Hart Lane na kufanikiwa kucheza hatua ya makundi ya Ubingwa wa Ulaya kwa mara ya kwanza tangu msimu wa mwaka 1961-62.

Kuna kila dalili Tottenham wakapangwa kundi moja na mabingwa watetezi Inter Milan ama Barcelona, lakini Redknapp amejigamba hawahofii timu yoyote.

Amesema"Tupo tayari kukabiliana na yeyote, tumekwishafuzu hatua ya makundi tutapambana na yeyote bila kuogopa".

Mabao matatu yaliyofungwa Peter Crouch na moja la Jermain Defoe, yaliiwezesha Tottenham kulipa deni la kufungwa mabao 3-2 ugenini katika mechi ya awali na hivyo kuingia hatua hiyo kwa jumla ya mabao 6-3 dhidi ya timu ya Bern kutoka Switzerland.

Man U yabanwa, Newcastle yaangamiza




Brede Hangeland alilipa deni kwa timu yake baada ya kupiga mpira kwa kichwa uliozaa goli la kusawazisha, wakati Fulham ikicheza na Manchester United, kabla ya hapo Hangeland alikuwa amejifunga mwenyewe kuizawadia Man U goli la pili.

Wachezaji wa Fulham wakimpongeza Brede Hangeland baada ya kuipatia timu yake goli la kusawazisha na kuokoa pointi moja.

Matokeo hayo yamevuruga mipango ya Manchester United kupata ushindi wa pili mfululizo tangu kuanza kwa michuano ya ligi kuu msimu huu.

Awali, kunako dakika ya 10 kipindi cha kwanza, Paul Scholes alitandika mkwaju wa mita 25 kuipatia United goli la kuongoza, ingawa Simon Davies alisawazisha kutoka miguu 12.

Katika shambulio kali la United, Hangeland alijifunga mwenyewe wakati kona ilipomzidia na United wakawa mbele kwa magoli mawili.

Hata hivyo United watajilaumu wenyewe kwa kushindwa kutumia penati ambayo ilipigwa na Nani kisha kupanguliwa na mlinda mlango David Stockdale dakika chache baadaye.

Hangeland aliruka juu kwa nguvu kudonyoa mpira wa kona na kuiwezesha United kuondoka na pointi moja.
Newcastle United dhidi ya Aston Villa

Katika mechi ya kwanza kati ya mbili siku ya Jumapili, Newcastle United waliorejea upya Ligi Kuu ya Soka ya England, walitoa kipigo cha mwizi kwa kuitandika Aston Villa magoli 6-0.

Villa ambao waliondokewa na kocha Martin O'Neil siku chache kabla ya msimu kuanza, walizidiwa kwa kila hali na kuwapa nafasi Newcastle kung'ara kwa kiasi kikubwa na kuondoa machungu ya kupoteza mechi ya kwanza dhidi ya Man United juma lililopita.

Katika mpambano huo, Andy Carroll alifunga magoli matatu wakati Kevin Nolan alifunga mawili.

Ukali wa washambuliaji wa Villa ulisababisha penati katika dakika ya tisa, lakini John Carew alipaisha mkwaju wake na baada ya hapo ikawa zamu ya Newcastle kuiangamiza Villa.

Wafungaji.

* Barton 12
* Nolan 31
* Carroll 34
* Carroll 67
* Nolan 87
* Carroll 90+3

Maaskari watatu wa zamani raia wa Marekani waliokatwa viungo vyao vya mwili wamepanda mlima Kilimanjaro

Kirk Bauer, Neil Duncan na Dan Nevins

Maaskari watatu wa zamani raia wa Marekani waliokatwa viungo vyao vya mwili wamepanda mlima Kilimanjaro, wakistahamili maporomoko na majeraha kufikia kilele cha mlima mrefu barani Afrika kila mmoja akiwa na mguu mmoja tu ambao ni imara.

Watu hao kutoka Vietnam, Afghanistan na Iraq, walikwea hadi kufikia juu ya mlima huo wenye urefu wa mita 5,891 uliopo nchini Tanzania.

Iliwachukua siku sita kufikia kileleni kwa nia ya kuonyesha kuwa ulemavu haumaanishi huna uwezo wa kufanya lolote.

Safari hiyo huchukua siku tano hadi sita, na ilibidi watu hao kusimama mara kwa mara ili kurekebisha miguu yao ya bandia, baada ya kuteleza sana.

Wakweaji hao wa mlima ni Dan Nevins, mwenye umri wa miaka 37, ambaye alipoteza miguu yake nchini Iraq, Neil Duncan, wa miaka 26, alipoteza miguu yote miwili katika shambulio la bomu lililotegwa barabarani Afghanistan mwaka 2005; na Kirk Bauer, mwenye miaka 62, aliyepoteza mguu mmoja huko Vietnam mwaka 1969.

Bw Bauer aliliambia shirika la habari la AP, " Ikiwa watu watatu waliokatwa viungo kutoka vita vitatu tofauti na kutoka vizazi tofauti na wana mguu mmoja tu wanaweza kupanda mlima Kilimanjaro, marafiki zetu wengine walemavu wanaweza kutoka na kupanda mlima au kuendesha basikeli au kuogelea, na wanaweza kuwa na maisha yenye afya njema."

Bw Nevis alipata jeraha katika kigutu ya moja ya miguu yake hiyo ya bandia na baada ya kufika kileleni aliondoshwa kwa kutumia machela.

Bw Bauer ni mkurugenzi mtendaji wa michezo ya walemavu wa Marekani, shirika lililopo mjini Wasington DC linaloshughulika na uzima wa afya na ushiriki wa michezo kwa walio na ulemavu.

Wednesday, August 18, 2010

Matokeo Ligi Kuu ya England


Wolverhampton 2-1 Stoke









Tottenham 0-0 Man City










Sunderland 2-2 Birmingham







Bolton 0-0 Fulham










Blackburn 1-0 Everton

Matokeo Ligi Kuu ya England


Katika mechi ya kufungua msimu, Tottenham Spur wakicheza uwanja wa nyumbani, walilazimishwa sare ya 0-0 na Manchester City.
Squad sheets: Aston Villa v West Ham United





Aston Villa ilipata ushindi wa magoli 3-0 dhidi ya West Ham walioonekana kukosa mwelekeo na kuelewana katika mechi yao ya kwanza msimu huu.

Kwa muhtasari matokeo yalikuwa hivi kwa mechi za mwanzo siku ya Jumamosi:-

Aston Villa 3-0 West Ham
Blackburn 1-0 Everton
Bolton 0-0 Fulham
Sunderland 2-2 Birmingham
Tottenham 0-0 Man City
Wigan 0-4 Blackpool
Wolverhampton 2-1 Stoke



Premier League
Aston Villa 0-0 West Ham
Stadium Villa Park
Sun, 17 Jan 2010
kick off:13:30 GMT
Referee: Mike Jones

squads
Aston Villa: Friedel, L Young, Cuellar, Dunne, Warnock, A Young, Milner, Petrov, Downing, Heskey, Agbonlahor, Guzan, Sidwell, Carew, Delph, Reo-Coker, Beye, Albrighton, Delfouneso.

West Ham United: Green, Kurucz, Faubert, Da Costa, Upson, Tomkins, Daprela, Spector, Kovac, Noble, Parker, Collison, Behrami, Payne, Diamanti, Jimenez, Stanislas, Nouble, Sears.
Aston Villa
Suspended: None Doubtful: None
Injured/unavailable: Bouma (toe), Davies (shoulder), Salifou (leave of absence)
West Ham
Suspended: None Doubtful: Noble & Parker (both hamstring)
Injured: Boa Morte, Cole & Hines (all knee), Davenport (leg), Dyer, Gabbidon & Ilunga (all hamstring), Franco (unspecified)
L A S T 6 M A T C H E S
Aston Villa West Ham
29.12 Aston Villa – Liverpool 0 : 1 29.12 Tottenham – West Ham 2 : 0
27.12 Arsenal – Aston Villa 3 : 0 27.12 West Ham – Portsmouth 2 : 0
19.12 Aston Villa – Stoke City 1 : 0 19.12 West Ham – Chelsea 1 : 1
15.12 Sunderland – Aston Villa 0 : 2 15.12 Bolton – West Ham 3 : 1
12.12 Manchester Utd – Aston Villa 0 : 1 12.12 Birmingham – West Ham 1 : 0
05.12 Aston Villa – Hull City 3 : 0 05.12 West Ham – Manchester Utd 0 : 4
Squad sheets: Aston Villa v West Ham United

Squad sheets: Aston Villa v West Ham United

Head-to-head
West Ham have won only one of their last 12 visits to Villa Park (W1, D6, L5). That was in January 2006 when Marlon Harewood scored the decisive penalty in a 2-1 Premier League victory.
Villa lost to West Ham for the first time in seven matches in November’s reverse fixture.

LEADING GOALSCORERS
Aston Villa
Agbonlahor: 9 goals (8 league); Milner: 7 goals (4 league)
West Ham
Cole: 7 goals (7 league); Diamanti: 6 goals (5 league)

MOST RECENT MEETING
West Ham 2-1 Aston Villa (4 November 2009)
West Ham scorers: Noble 45 pen, Hines 90.
Aston Villa scorer: A Young 52.

17′ Radoslav Kovac
77′ Jack Collison
89′ Stilian Petrov
89′ Junior Stanislas

Tuesday, August 17, 2010

Kesi ya UKIMWI: 'Naomba radhi'

Mwimbaji wa kundi moja la muziki nchini Ujerumani lijulikanalo kama No Angels, amekiri kosa la kufanya mapenzi bila kinga na wanaume kadhaa bila kuwaonya kuwa ana virusi vya HIV.
Nadja Benaissa

Nadja Benaissa

Mwanamuziki huyo Nadja Binaissa mwenye umri wa miaka 28,


alikuwa akizungumza katika ufunguzi wa kesi yake katika mji wa Darmstadt nchini Ujerumani.
Ninaomba radhi

"Ninaomba sana radhi", Bi. Benaissa ameiambia mahakama. Hata hivyo amekanusha kuambukiza mtu yeyote kwa makusudi.

Anakabiliwa na mashitaka ya kudhuru mwili kwa kutuhumiwa kumuambukiza mtu mmoja virusi.

Aidha, ameshitakiwa kwa tuhuma za kutaka kudhuru mwili wa mtu kwa kutuhumiwa kufanya mpenzi na wanaume wawili ambao hata hivyo hawakuambukizwa.

Iwapo atakutwa na hatia, Bi. Benaissa huenda akakabiliwa na kifungo cha kati ya miezi sita hadi miaka 10.
Mapenzi bila kinga

Baada ya kesi kufunguliwa, shirika la habari la Ujerumani DAPD liliandika taarifa kutoka kwa mwanasheria wa Bi. Benaissa, ikisema mwanamuziki huyo hakuweza kushughulikia vyema suala la kuishi na virusi vya HIV, na pia kukiri kufanya mapenzi bila kutumia kinga.

Lakini mwimbaji huyo alisema: " Hata mara moja sikutaka mpenzi wangu kuambukizwa."

Bi. Benaissa alikamatwa mjini Frankfurt mwaka jana, muda mfupi kabla ya kufanya onyesho lake la muziki, na aliwekwa rumande kwa siku 10.
Uhalifu wa maambukizi

Wanaharakati wa masuala ya UKIMWI wameshutumu mamlaka za huko kwa jinsi walivyolishughulikia suala la kukamatwa kwa msanii huyo, na kuonya dhidi ya kuharakisha suala la uhalifu wa maambukizi ya virusi vya HIV.

Kwa mujibu wa waendesha mashitaka, Bi. Benaissa alijijua kuwa na virusi vya HIV tangu mwaka 1999.

Mpenzi wake wa zamani, ambaye ana virusi vya HIV, anasema mwimbaji huyo alimuambukiza mwaka 2004, na anatazamiwa kufika mahakamani mjini Darmstadt kama mlalamikaji.

Mwezi Novemba mwaka jana, Bi. Benaissa katika tamasha la UKIMWI mjini Berlin, alijitokeza na kusema hadharani : "Jina langu ni Nadja Benaissa, nina miaka 27, nina mtoto wa kike na ninaishi na virusi vya HIV."
Mafanikio

Kundi la waimbaji la No Angels liliundwa mwaka 2000 katika kipindi cha televisheni cha waimbaji wa kimataifa, na baadaye kurekodi vibao vilivyovuma na hatimaye kuwa kundi la kina dada lenye mafanikio zaidi nchini humo.

Mwaka 2007, waimbaji hao waliungana tena na kushiriki katika mshindano ya wimbo bora wa Eurovision, na kushika nafasi ya 23.

Kesi ya Bi. Benaissa inatarajiwa kumalizika mwisho wa mwezi huu.