Saturday, July 24, 2010

Lundega: Miss Tanzania mwaka huu balaa


Hayo yamesemwa na Mkurugenzi wa Kampuni ya Lino Agency ambayo ndiyo waandaaji wa mashindano hayo, Hashimu Lundenga 'Uncle Hashimu'.

Akizungumza jijini Dar es Salaam juzi, Lundenga alisema kuwa tofauti na miaka yote, mwaka huu kila sehemu wamejitahidi kutoa warembo wenye sifa za urembo hivyo kuongeza ushindani zaidi.

"Tulivyoona tu katika mikoa ambayo imeshapata wawakilishi wao, kuna warembo wengi wenye vigezo haswa vya kutwaa taji hili, kwa hiyo hatujui ni mkoa upi hasa mwaka huu utatwaa taji hilo," alisema Lundenga.

Mwaka jana mkoa wa Mwanza ndiyo ulioibuka kidedea baada ya mlimbwende wake Mariamu Gerald kuibuka kidedea na kutwaa taji hilo.

No comments:

Post a Comment