Saturday, July 24, 2010

Mimi ni Kidum .Nataka kutoa maelezo

Mimi ni Kidum .Nataka kutoa maelezo kikamilifu kuhusiyana na iyi muzozo wa uyu wimbo wangu na Lady Jaydee .Hakuna shida yeyote yipo kati yangu na Hermy B ambayo ni producer wa round ya kwanza ya recording ya uyu wimbo .

Kama vile munajuwa mimi naishi nairobi na hapa ndipo nafanya shuhuli za muziki wangu kwa muda mrefu .Sasa kama kwa mfano nime rekodi Dar es salaam alafu nisikiye kuna hitirafu kidogo kwa wimbo ni ngumu niwe nachukuwa ndege kila mara nikikuja Dar es salaam ingawa napapenda sana wakati hapa nairobi piya kuna studios .

Kwa mfano version ya kwanza Key ile tuliimbiya mimi na jaydee ni yenye ambao ilikuwa chini sana kuweza kuwa rahisi kwa mwana dada lakini tulipo rudiya sasa mwana Dada sauti yake ikatoka kama ya malaika .Hapakuwa ubaya wakurudiya ku rekodi tena uyu wimbo sababu mimi mwenyewe niko msanii na kuna kile kitu mimi natafuta kwa hali ya ubora zaidi kama sikipati bila shaka ata ku rekodi mara ya tatu siwezi kusita kufanya . Wimbo ni wangu mimi na lady jaydee sisi wenyewe tukielewana na tu amuwe kuwurudiya sioni kama kuna ubaya .
Hata Hermy B mwenyewe na amini munamusemeya uwongo ya kwamba anamatatizo kuhusiyana uyu wimbo sababu mimi mwenyewe naelewa vema kwenye radio stations nyingi wanacheza version yake ya Audio . bado ni uyo wimbo tu iwe video ama audio .Na pia bado ni Kidum na Lady Jaydee iwe ni video ama ni Audio

No comments:

Post a Comment