Tuesday, July 20, 2010

Mrembo wa Temeke Apatikana


Fainali za mashindano hayo ziliwashirikisha jumla ya warembo kumi na mbili.

Mkurugenzi wa Shindano hilo katika Wilaya ya Temeke Ben Kisaka alisema kuwa kutokana na maandalizi mazuri walivyofanya wana uhakika kuwa mwaka huu Miss Tanzania atatoka katika wilaya hiyo.

Katika shindano hilo kivutio kikubwa kilikuwa ni kwa baba na mwana Banana Zorro na Zahiri Zorro ambao wote walikuwa kivutio kikubwa pale walipoimba pamoja jukwaani.

Mshindi wa pili katika shindano hilo alikuwa ni Anna Daudi na nafasi ya tatu ilichukuliwa na Britney Urassa nafasi ya nne ilikwenda kwa Domitria Innocent na watano alikuwa Ritta Samuel.

Washiriki wote watashiriki katika kambi ya Miss Tanzania ambayo itaanza hivi karibuni baada ya kumalizika kwa mashindno ya umiss ya mikoa na kanda.

No comments:

Post a Comment